Wednesday, September 30, 2020
UN yamuunga mkono Magufuli kutokomeza ukatili wa mwanamke Ikungi
Saturday, September 12, 2020
Mkuu wa kitengo cha wateja wa rejareja wa Benki ya I&M, Lilian Mtali akifafanua jambo wakati wa kikao cha wateja kilichofanyika ijumaa 11 septemba Hoteli ya Golden Tulip Masaki
.......................................................................
Benki ya I&M Tanzania leo 11 septemba 2020 imekutana na wateja wake katika Hotel ya Golden Tulip kama ilivyo ada ya Benki ya I&M Tanzania kukutana na wateja wake kwaajili ya kujadiliana mada mbalimbali zinazohusiana na huduma za kibenki, changamoto na njia za kuwapatia wateja wake suluhisho ili wafurahie huduma za benki yao.
Akiongea kwenye kikao hicho, Baseer Mohammed Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo alisema, “Kwaniaba ya wafanyakazi wote wa Benki ya I&M napenda kuwashukuru wateja wetu wote mlioweza kuitikia wito na kuhudhuria kikao hiKi kifupi chenye mada zenye tija kwa maendeleao ya benki na wateja kwa ujumla. Hiki kikao kwaajili yenu hivyo msisite kuuliza maswali na kuchangia mada zitakazoleta maboresho makubwa kwenye huduma zetu.
Mkuu wa kitengo cha wateja wa rejareja, Lilian Mtali pia aliongezea kwa kusema, “hiki kikao ni muhimu sana kwetu kwani tunategemea sana mrejesho wenu kuhusiana na huduma zetu na wapi tuboreshe ili kuhakikisha tunawapa huduma bora sana. Tunashukuru sana kwa mawazo yenu, maoni kuhusu maboresho pia pongezi mlizotupa tunawaahidi tutafanya Zaidi ili kuhakikisha I&M ni benki pekee ambayo mtakua mkiifikiria mtakapohitaji huduma bora za kibenki.
Wateja pia hawakua mstari wa nyuma kwani walifurahia sana ukaribu ambao benki hiyo umeweka kukutana na wateja wao na kuhakikisha wanapata huduma bora Zaidi na za kisasa za kibenki. Wameipongeza benki ya I&M kwa huduma bora, uharaka katika kujibu changamoto za wateja, pia mifumo ya kidijitali kuhakikisha wateja wanapata huduma saa 24 kupitia iClick, na huduma za kibenki kwa njia ya simu *150*32#.
Mbali na matawi yaliopo Dar es salaam Nyerere, Maktaba, Tawi kuu, Kariakoo na Oysterbay, benki ya I&M pia ipo Moshi, Arusha na Mwanza na muda si mrefu inaanzisha huduma za wakala maeneo mbalimbali na mikoa mbalimbali ili kufikisha huduma kwa haraka.
Friday, September 4, 2020
WORLD VISION YAWANOA WANAHABARI KUHUSU LISHE NA AFYA YA UZAZI
Meneja wa Mradi wa ENRICH, Bi Mwivano Malimbwi (aliyesimama) akitoa mafunzo maalum ya malengo ya mradi huo ya utoaji wa elimu ya lishe na kuboresha afya ya uzazi kwa vijana balehe kwenye mikoa ya Singida na Shinyanga kwa waandishi wa habari ya Mkoa wa Singida (hawapo pichani)
leo, aliyekaa ni mtaalam wa Jinsia na Utetezi wa Mradi Huo Tumaini
Fred
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi akiangalia mazao ya asali na mashine ya kukamulia asali ya kikundi cha ufugaji wa nyuki mkoani Singida kinachofadhiliwa wa World Vision hivi karibuni
Na. John Mapepele,Singida
Shirika la World Vision nchini limewataka waandishi wa habari kama wadau wakuu wa Shirika hilo kutoa taarifa sahihi za kazi za shirika hilo kwenye mradi wake wa ENRICH ambao unatekelezwa katika mikoa ya Singida na Shinyanga.
Mradi huo unalengo la kupeleka elimu ya lishe na afya ya uzazi kwa vijana balehe vijijini ili kupunguza vifo vya akinamama wajawazito na watoto chini ya siku 1000 na ili kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano ili kuboresha maisha ya watanzania.
Akitoa mafunzo maalum kuhusu malengo wa mradi kwa waandishi wa Mkoa wa Singida , Meneja wa Mradi wa ENRICH Bi, Mwivano Malimbwi amesema mradi huu ni wa miaka mitano kuanzia mwaka 2016 hadi mwaka 2021 na umejikita katika kuwezesha huduma za lishe ili kuimarisha afya ya mama na mtoto kwa gharama za dola milioni 8.4 za kikanada.
Kwa mujibu wa Malimbwi malengo mahususi ya ENRICH ni kupunguza vifo vya akina mama na watoto kwa kuangalia visababishi vya vifo hivyo ambapo mradi umeelekeza nguvu kwenye kuimarisha mifumo ya utoaji wa afya katika vituo vya kutolea huduma hizo.
Aliongeza kuwa awali wakati mradi ulipoanza walibaini changamoto ya upatikanaji wa vifaa vya kumchunguza hali ya kiliishe ya mtoto vilikuwa na upungufu mkubwa ambapo vituo vichache vilikuwa na vifaa hivyo vya kupimia urefu na mzingo wa kati wa mkono kwa akina mama na mtoto
Alisema kuwa watoa huduma wachache walipata mafunzo ya afya ya lishe kwenye ngazi ya mkoa na wilaya ambapo hakukuwa na watoa huduma katika maeneo ya vijijini.
Aidha alisema pia hakukuwa na elimu ya uongozi kwenye kamati za afya za mikoa na wilaya ambapo Mradi uliwajengea uwezo ili kuwa sehemu ya kuleta mabadiliko kwa pamoja badala ya kuwa watoa maamuzi.
Aidha mipango na bajeti ilikuwa ikifanywa kwa hisia badala ya kutumia takwimu sahihi.
Malimbi amesema lengo la pili la Mradi ni kuongeza uzalishaji wa chakula chenye uwingi wa virutubisho ambapa kwenye eneo hili amessisitiza kuwa mkakati umekuwa katika kuongeza uzalishaji ulioongezwa kibailojia, kuongeza utumiaji wa virutubishi kwa watoto na sayansi ya ulaji na ufyonzaji wa virutubishi,
Alisema pia katika mikoa ya Singida na Shinyanga imebarikiwa kuwa na vyakula vya makundi yote na matunda ya asili kama sasati, rade na furu ambayo kama yakitumika kikamilifu yatasaidia sana kuboresha lishe na kupunguza udumavu kwa watoto.
Alipongeza jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Dk. Rehema Nchimbi kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa suala la lishe na afya ya uzazi vinakuwa kipaombele cha kwanza kwa wananchi ambapo pia amesema amehamasisha ulaji na ulimaji wa viazi lishe na kuwafanya wananchi wa Mkoa wa Singida tofauti na awali ambapo vilikuwa vikiuzwa nje ya Mkoa.
Aidha amesema Mradi umehamasisha akina mama kulima bustani za mbogamboga kwenye kila kaya ili kuhakikisha kuwa kwenye kila mlo mboga zinakuwepo.
Amesema lengo la mwisho la mradi huo ni kuhakikisha kuwa kunakuwa na uwajibikaji wa wadau wote muhimu na kila mmoja anafanya majukumu yake kwa ufasaha, ambapo ametolea mfano kuwa Serikali kama mdau mkuu ina wajibu wa kuweka vituo vya kutolea huduma na mtoa huduma ambapo jamii inawajibu wa kuvitumia vituo hivyo na watoa huduma.
Mradi wa ENRICH ni Mradi wenye sekta nyingi na unafadhiliwa na Serikali ya nchi ya Canada ambapo unatekelezwa kwa kushirikiana na wabia ambao ni Nutritional International, Canadian Society for International Health anayejikita katika kuimarisha mfumo wa afya.
Ikiwemo Harvest Plus, kwenye Sekta ya Kilimo, Chuo kikuu cha Toronto katika kufanya tathimini na ufuatiliaji wa mradi na World Vision ambaye ni msimamizi mkuu wa fedha wa mradi huo. Serikali ya Tanzania ni mtekelezaji namba moja chini ya TAMISEMI.






