Wednesday, September 30, 2020

UN yamuunga mkono Magufuli kutokomeza ukatili wa mwanamke Ikungi

 

   Picha ya pamoja ya Mkuu wa mkoa wa Singida  Dk. Rehema Nchimbi(mwenye kilemba) na       wawakilishi wa mashirika ya kimataifa na wadau mbalimbali wa maendeleo mara baada ya uzinduzi wa mradi
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk Rehema Nchimbi(kulia) akiwa na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Nchini Tanzania, Zlatan Milisic baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa mradi
 

 Na John Mapepele, Ikungi
 MKUU wa  Mkoa wa Singida Mhe, Dk. Rehema Nchimbi  leo amezindua  miongoni mwa miradi mikubwa iliyowahi kutekelezwa nchini, mradi wa  pamoja  baina ya Mashirika ya Kimataifa ya UN Women na UNFPA kupitia ufadhiri  wa  Shirika la KOICA wa Tuufikie usawa  wa jinsia kupitia kuwawezesha wanawake na wasichana utakaogharimu takribani bilioni 11.5 za kitanzania  ambao utatekelezwa  katika Wilaya ya Ikungi mkoani Singida na Msalala mkoani  Shinyanga katika kipindi cha  miaka mitatu kuanzia sasa.
 Dk. Nchimbi amesema lengo kuu la mradi huo ni kuchangia  katika kuwawezesha  wanawake na wasichana  kuwakwamua kiuchumi na kijamii katika mikoa ya Singida na Shinyanga  ili kufikia usawa wa kijinsia ambapo amewataka watendaji wote wa Serikali ambao watatekeleza mradi huo kuwa makini katika utekelezaji wa mradi ili  malengo ya mradi huo yaweze kufikiwa.

Amesisitiza kuwa Serikali haitasita kuwachukulia hatua kali watendaji ambao  kwa namna moja au nyingine hawataendana na kasi ya utekelezaji wa miradi chini ya Serikali ya awamu ya Tano  inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli ambapo amesema  mrai huo  ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi  ili kuwaletea wananchi  maendeleo ya  kweli.

Kwa mujibu wa  Mkurugenzi wa  KOICA  Tanzania, Bi Jieun Mo,  walengwa wasio wa moja kwa moja takribani  wakazi 40,000 kutoka kwenye wilaya  ya Ikungi na Msalala na walengwa  wa moja  kwa moja 2350 wanawake na wasichana  kutoka katika wilaya hizo watanufaika na mradi huu ambapo pia  wanaume na wanawake 6000 wa Wilaya  ya Ikungi watanufaika kwenye eneo la muingiliano wa  hati za ardhi.

Mo ameainisha kuwa  shughuli za mradi katika kuwaweza wanawake  kwenye eneo la uchumi zitajikiza zaidi kwenye kuimarisha uwezo wa wanawake  na vijana   wakulima ili waweze kutumia  njia nzuri za kilimo na hali ya hewa katika uzalishaji wa alizeti na kilimo cha bustani, kukuza uuzaji wa pamoja, ujuzi wa ujasiriamali na wakala wa uchumi  wa wanawake  na kuimarisha  usalama wa ardhi na umiliki.

Amesisiza kuwa  shughuli hizo zitatekelezeka  kupitia kuunda  vikundi vya uzalishaji wa kilimo cha bustani kwa wanawake, kuunganisha  wanunuzi wa vikundi  vya wakulima vya wanawake,kusaidia ujenzi wa  ghala kubwa  moja la alizeti na kituo cha ukusanyaji kilomo cha bustani ili  kuboresha uuzaji wa pamoja na utunzaji baada ya kuvuna, kutoa mafunzo ya ujasiriamali, kutoa mafunzo ya ujasiriamali na ufikiaji wa habari za kifedha na kufuatilia ushauri wa usimamizi wa biashara na  fedha na kukuza  umiliki wa ardhi pekee na wa pamoja  wa wanawake kupitia utoaji wa  Hati za Haki za kimila za Makaazi(CCROs).

Mwakilishi wa UN Women  Bi, Hodan Addou ameishukuru Serikali  ya  Tanzania  kuwa ushirikiano wake katika kuhakikisha  kuwa mradi huu  hatimaye umeanza kutekelezwa ambapo amesema Shirika lake  linaunga mkono juhudi za Serikali za kumkomboa mwanamke ili kuondokana na  unyanyasaji wa kijinsia.

Bi Addou amesisitiza kuwa mradi utasaidia uwezeshaji kijamii kwa kuwawezesha  wanawake kusimamia haki zao, kujenga ujuzi wa ujasiiamali wa wanawake na wasichana kukabiliana  na unyanyasaji wa kijinsia na kuimarisha mifumo ya kuzuia na kukabiliana na unyanyasaji wa kijinsia kupitia kuanzisha na kuandaa vifaa katika madawati matatu ya  Polisi ya Jinsia na Watoto, kuanzisha  vituo vitatu vya  huduma  ya dharura katika  vituo vya wilaya, kuunda nafasi salama ya umma, kujenga uwezo  wa nambari ya msaada ya watoto kitaifa, kuunda na kuimarisha Klabu za Wasichana na kuunda Kamati za ulinzi na ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Nchini Tanzania  Zlatan Milisic   ameipongeza Serikali kwa kuwa  na mradi huo na kuongeza kuwa mradi huo unaendana na malengo ya endelevu ya 2030 hususani lengo namba 5 kuhusiana kuwaendeleza wanawake  katika nyanja mbalimbali na kuongeza kuwa mwaka 2020 ni mwaka muhimu sana kwa kuwa tunaelekea  katika kutimiza miaka 25 ya azimio la wanawake la Beijing.

Ameeleza kuwa  malengo endelevu ya 2030 yameeleza kuwa ili kufikia maendeleo ya nchi kumtambua mwanamke ni jitihada muhimu sana  katika kuharakisha na kutimiza malengo yote ya maendeleo ambapo ameihakikishia Serikali ya Tanzania kuendelea kufanya kazi kwa karibu sana  ili kuhakikisha wanawake wanakuwa chachu ya maendeleo katika  nchi ya Tanzania.

Mwakilishi wa UNFPA, Dk. Winfred amesema kuwa uzinduzi wa mradi umelenga kutokomeza aina zote za unyanyasaji wa kijinsia  na kuimarisha usawa katika jamii ikiwa ni pamoja na  kuimarisha maisha ya wanawake ambapo amesisitiza kitovu cha matatizo ya kijinsia  ni wanaume na mila na desturi potofu zinazomtazama mwanamke kwa kumdharirisha hivyo juhudi za makusudi  zinatakiwa  kufanywa za kuwaweka wanaume mbele ili kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake.

Naye  Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Edward Mpogolo  amesisitiza kuwa kazi nzuri zinazofanywa na  Rais John Pombe Magufuli katika Nyanja mbalimbali ndiyo zinazoyafanya  jumuiya za kimataifa  kuunga mkono kwa kutoa  misaada  kupitia miradi mbalimbali hapa nchini

Saturday, September 12, 2020

 

Timu ya wafanyakazi wa I&M Bank ikiongozwa na mtendaji Mkuu wa Benki hiyo Bw. Baseer Mohammed, wakuu wa idara mbalimbali, meneja wa matawi ya Dar es salaam pamoja na wateja katika picha ya pamoja baada ya kumaliza kikao hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam.
Mtendaji Mkuu wa Benki ya I&M, Bw. Baseer Mohammed akiongea na wateja wakati wa kikao kifupi na wateja Golden Tulip siku ya Ijumaa 11 Septemba.
Mkuu wa kitengo cha wateja wa rejareja wa Benki ya I&M,  Lilian Mtali akifafanua jambo wakati wa kikao cha wateja kilichofanyika ijumaa 11 septemba Hoteli ya Golden Tulip Masaki

.......................................................................

Benki ya I&M Tanzania leo 11 septemba 2020 imekutana na wateja wake katika Hotel ya Golden Tulip kama ilivyo ada ya Benki ya I&M Tanzania kukutana na wateja wake kwaajili ya kujadiliana mada mbalimbali zinazohusiana na huduma za kibenki, changamoto na njia za kuwapatia wateja wake suluhisho ili wafurahie huduma za benki yao. 

Akiongea kwenye kikao hicho, Baseer Mohammed Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo alisema, “Kwaniaba ya wafanyakazi wote wa Benki ya I&M napenda kuwashukuru wateja wetu wote mlioweza kuitikia wito na kuhudhuria kikao hiKi kifupi chenye mada zenye tija kwa maendeleao ya benki na wateja kwa ujumla.  Hiki kikao  kwaajili yenu hivyo msisite kuuliza maswali na kuchangia mada zitakazoleta maboresho makubwa kwenye huduma zetu.

Mkuu wa kitengo cha wateja wa rejareja, Lilian Mtali pia aliongezea kwa kusema, “hiki kikao ni muhimu sana kwetu kwani tunategemea sana mrejesho wenu kuhusiana na huduma zetu na wapi tuboreshe ili kuhakikisha tunawapa huduma bora sana. Tunashukuru sana kwa mawazo yenu, maoni kuhusu maboresho pia pongezi mlizotupa tunawaahidi tutafanya Zaidi ili kuhakikisha I&M ni benki pekee ambayo mtakua mkiifikiria mtakapohitaji huduma bora za kibenki.

Wateja pia hawakua mstari wa nyuma kwani walifurahia sana ukaribu ambao benki hiyo umeweka kukutana na wateja wao na kuhakikisha wanapata huduma bora Zaidi na za kisasa za kibenki. Wameipongeza  benki ya I&M kwa huduma bora, uharaka katika kujibu changamoto za wateja, pia mifumo ya kidijitali kuhakikisha wateja wanapata huduma saa 24 kupitia iClick, na huduma za kibenki kwa njia ya simu *150*32#.

Mbali na matawi yaliopo Dar es salaam Nyerere, Maktaba, Tawi kuu, Kariakoo na Oysterbay, benki ya I&M pia ipo Moshi, Arusha na Mwanza na muda si mrefu inaanzisha huduma za wakala maeneo mbalimbali na mikoa mbalimbali ili kufikisha huduma kwa haraka.

Friday, September 4, 2020

WORLD VISION YAWANOA WANAHABARI KUHUSU LISHE NA AFYA YA UZAZI

 


Meneja wa Mradi wa ENRICH, Bi Mwivano Malimbwi (aliyesimama) akitoa mafunzo maalum ya malengo ya mradi huo ya utoaji wa elimu ya lishe na kuboresha afya ya uzazi kwa vijana balehe kwenye  mikoa ya Singida na Shinyanga kwa waandishi wa habari ya Mkoa wa Singida (hawapo pichani)
leo, aliyekaa  ni mtaalam wa Jinsia na Utetezi wa Mradi Huo Tumaini
Fred


Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi akiangalia mazao ya asali na mashine ya kukamulia asali  ya kikundi cha ufugaji wa nyuki mkoani Singida kinachofadhiliwa wa World Vision hivi karibuni

Na. John Mapepele,Singida

Shirika la World Vision nchini  limewataka waandishi wa habari kama wadau wakuu wa Shirika  hilo  kutoa taarifa sahihi za kazi za  shirika hilo  kwenye mradi wake wa ENRICH  ambao unatekelezwa  katika  mikoa ya Singida na Shinyanga.

Mradi huo unalengo la kupeleka elimu ya lishe na afya ya uzazi kwa vijana balehe vijijini ili kupunguza  vifo vya akinamama wajawazito na watoto chini  ya siku 1000 na  ili kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano ili kuboresha maisha ya watanzania.

Akitoa mafunzo maalum  kuhusu malengo wa mradi kwa waandishi wa Mkoa wa Singida , Meneja wa Mradi wa ENRICH  Bi, Mwivano Malimbwi amesema mradi huu  ni  wa miaka mitano  kuanzia mwaka 2016 hadi mwaka  2021 na umejikita katika  kuwezesha  huduma za lishe ili kuimarisha afya  ya  mama na mtoto  kwa gharama za dola  milioni 8.4 za kikanada.

 Kwa mujibu wa Malimbwi  malengo  mahususi ya ENRICH ni kupunguza  vifo vya akina mama na watoto  kwa kuangalia  visababishi  vya vifo hivyo ambapo mradi umeelekeza nguvu kwenye kuimarisha mifumo ya utoaji wa afya katika vituo vya kutolea  huduma  hizo.

Aliongeza kuwa awali wakati mradi ulipoanza  walibaini  changamoto ya upatikanaji wa vifaa vya kumchunguza hali ya kiliishe ya mtoto  vilikuwa na upungufu mkubwa ambapo  vituo vichache  vilikuwa na  vifaa hivyo vya kupimia urefu na mzingo wa kati wa mkono kwa akina mama na mtoto

Alisema kuwa watoa huduma wachache walipata mafunzo ya afya ya lishe  kwenye ngazi ya mkoa na wilaya ambapo  hakukuwa na watoa huduma katika maeneo ya vijijini.

Aidha alisema pia hakukuwa na elimu ya uongozi kwenye kamati za afya za mikoa  na wilaya ambapo Mradi uliwajengea uwezo ili kuwa sehemu ya  kuleta mabadiliko kwa pamoja  badala ya kuwa watoa maamuzi. 

Aidha mipango na bajeti ilikuwa ikifanywa kwa hisia  badala ya kutumia takwimu sahihi.

Malimbi amesema lengo la  pili  la Mradi ni kuongeza uzalishaji wa chakula  chenye uwingi wa virutubisho ambapa kwenye eneo hili amessisitiza kuwa mkakati umekuwa  katika kuongeza  uzalishaji ulioongezwa kibailojia, kuongeza utumiaji wa virutubishi kwa watoto na sayansi ya ulaji na ufyonzaji wa virutubishi,

Alisema pia katika mikoa ya Singida na Shinyanga imebarikiwa kuwa na  vyakula vya makundi yote na matunda ya asili kama sasati, rade na furu ambayo kama yakitumika kikamilifu yatasaidia sana kuboresha lishe na kupunguza udumavu kwa watoto.

Alipongeza jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Dk. Rehema Nchimbi  kuwa  mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa suala la lishe na afya ya uzazi vinakuwa kipaombele cha kwanza kwa wananchi ambapo pia amesema amehamasisha ulaji na ulimaji wa viazi lishe na kuwafanya wananchi wa Mkoa wa Singida tofauti na awali ambapo vilikuwa vikiuzwa nje ya Mkoa.

Aidha amesema Mradi umehamasisha akina mama kulima bustani za mbogamboga kwenye kila kaya ili kuhakikisha kuwa  kwenye kila mlo mboga zinakuwepo.

Amesema lengo la mwisho la mradi  huo  ni kuhakikisha  kuwa  kunakuwa na uwajibikaji wa wadau wote muhimu na kila mmoja anafanya majukumu yake kwa ufasaha, ambapo ametolea mfano kuwa Serikali kama mdau mkuu ina wajibu wa kuweka  vituo vya kutolea huduma na mtoa huduma ambapo jamii inawajibu wa kuvitumia vituo hivyo na watoa  huduma.

Mradi wa ENRICH ni Mradi wenye sekta nyingi na unafadhiliwa na Serikali ya  nchi ya Canada ambapo unatekelezwa kwa kushirikiana  na wabia ambao ni Nutritional International, Canadian Society for  International Health anayejikita katika kuimarisha mfumo wa afya.

Ikiwemo Harvest Plus, kwenye Sekta ya Kilimo, Chuo kikuu cha Toronto  katika kufanya tathimini na ufuatiliaji wa mradi na World Vision ambaye ni msimamizi mkuu wa fedha wa mradi huo. Serikali ya Tanzania ni mtekelezaji namba moja chini ya TAMISEMI.