Tuesday, May 11, 2021

WAFANYAKAZI WA BENKI YA I&M WAMETOA MSAADA WA VITU MBALIMBALI KATIKA KITUO CHA WATOTO YATIMA – KIGAMBONI, DAR ES SALAAM.

 

Wafanyakazi wa Benki ya I&M wakiwa na baadhi ya watoto wa kituo hicho
Bi.Anitha Pallangyo, meneja masoko Benki ya I&M wapili kushoto akikabidhi baadhi ya zawadi walizopeleka kwenye kituo hicho cha watoto yatima
Timu ya Benki ya I&M leo walipotembelea kituo cha yatima chini ya mpango wao wa kujitolea wa 'IM for You' kushoto ni Bi. Hellen Mbwana, afisa wa benki kitengo cha ukaguzi, Anitha Pallangyo, meneja masoko, Mlekwa Augustine, huduma kwa wateja, Theresia Nguma kitengo cha malipo, fedha na biashara, na Debora mwakyoma afisa masoko na mawasiliano ya benki.

 Timu ya wafanyakazi wa I&M walipotembelea kituo cha watoto yatima cha Lady Fatema kilichopo Mjimwema mageti saba, kigamboni Jijini Dar es salaam.

DAR ES SALAAM. Wafanyakazi wa Benki ya I&M Tanzania siku ya Jumanne tarehe 11, Mei, 2021, wamejitolea msaada wa vitu mbalimbali kama vile vyakula, nguo, sabuni pamoja na vifaa vya shule katika moja ya kituo cha kulea watoto yatimakiitwacho ‘Lady Fatema’  kilichopo Mjimwema mageti saba, Kigamboni Jijini Dar es salaam chini ya mpango wao wa ‘IM FOR YOU’ katika jitihada za kurudisha kwa jamii kupitia mpango huo ambapo wafanyakazi hujitolea kwa jamii kwa njia mbalimbali kama vile kutoa elimu ya fedha na ujasiriamali kwa wanawake na vijana ili waweze kujiajiri pamoja na kusaidia vitu mbalimbali kwa wahitaji.

Wasimaizi wa kituo hicho Bi. Mariam Ramadhan na mmewe Bw. Kalekela Omari Mahmood walianzisha kituo hicho mnamo mwaka 2011 wakiwa na lengo la kusaidia watoto yatima wanaoishi katika mazingira hatarishi wakiwapatia elimu, chakula na hifadhi ya kulala. Mbali na misaada mbalimbali inayopelekwa na wafadhili, kituo hicho kina changamoto ya eneo la kutosha la kuweza kuhifadhi watoto wengi na wa jinsia tofauti kwani kwa sasa imewalazimu kubaki na jinsia ya kiume tu kutokana na ukosefu wa vyumba vya kutosha kwaajili ya watoto hao.

Katika kuadhimisha mwezi mtukufu wa Ramadhani na ikiwa ni wiki ya kuelekea sikukuu ya Eid Al-Fitr, wafanyakazi wa benki ya I&M waliamua kujitolea vitu hivyo katika kituo cha kulea watoto yatima Mjimwema Kigamboni ili na wao waweze kusheherekea na kufurahia sikukuu ya EID inayotarajiwa kuwa mwishoni mwa wiki hii kutegemeana na kuandama kwa mwezi. Vilevile wafanyakazi wa benki ya I&M waliweza kuwapa elimu ya usimamizi wa fedha na ujasiriamali kwa vijana na wanawake waliokuwa katika kituo hicho ili iweze kuwasaidia katika usimamizi wa fedha za kituo hicho pamoja na kijiajiri wao wenyewe pindi watakapoanza kujitegemea.

Benki ya I&M kupitia wafanyakazi wake wameweza kufanya kampeni mbalimbali za kusaidia jamii kama vile kujitolea kwa kufundisha wanawake, vijana na wajasiriamali katika kikundi cha Wanawake wajasiriami kilichopo Yombo vituka, Temeke jijini Dar es salaam, vilevile wiki iliyopita wafanyakazi wa benki hiyo walijitolea damu  ili kusaidia wagonjwa wenye uhitaji wa damu katika hospitali ya Taifa ya Muimbili.

WAFANYAKAZI WA BENKI YA I&M WAMETOA MSAADA WA VITU MBALIMBALI KATIKA KITUO CHA WATOTO YATIMA – KIGAMBONI, DAR ES SALAAM

 

Bi.Anitha Pallangyo, Meneja Masoko Benki ya I&M wapili kushoto akikabidhi baadhi ya zawadi walizopeleka kwenye kituo hicho cha watoto yatima
Timu ya Benki ya I&M leo walipotembelea kituo cha yatima chini ya mpango wao wa kujitolea wa 'IM for You' kushoto ni Bi. Hellen Mbwana, afisa wa benki kitengo cha ukaguzi, Anitha Pallangyo, meneja masoko, Mlekwa Augustine, huduma kwa wateja, Theresia Nguma kitengo cha malipo, fedha na biashara, na Debora mwakyoma afisa masoko na mawasiliano ya benki.

Timu ya wafanyakazi wa I&M walipotembelea kituo cha watoto yatima cha Lady Fatema kilichopo Mjimwema mageti saba, kigamboni Jijini Dar es salaam.


                  .............................................
DAR ES SALAAM. Wafanyakazi wa Benki ya I&M Tanzania siku ya Jumanne tarehe 11, Mei, 2021, wamejitolea msaada wa vitu mbalimbali kama vile Vyakula, Nguo, Sabuni pamoja na vifaa vya Shule katika moja ya Kituo cha kulea watoto yatima kiitwacho ‘Lady Fatema’  kilichopo Mjimwema mageti saba, Kigamboni Jijini Dar es salaam chini ya mpango wao wa ‘IM FOR YOU’ katika jitihada za kurudisha kwa jamii kupitia mpango huo ambapo wafanyakazi hujitolea kwa jamii kwa njia mbalimbali kama vile kutoa elimu ya fedha na ujasiriamali kwa wanawake na vijana ili waweze kujiajiri pamoja na kusaidia vitu mbalimbali kwa wahitaji.

Wasimaizi wa kituo hicho Bi. Mariam Ramadhan na mmewe Bw. Kalekela Omari Mahmood walianzisha kituo hicho mnamo mwaka 2011 wakiwa na lengo la kusaidia watoto yatima wanaoishi katika mazingira hatarishi wakiwapatia elimu, chakula na hifadhi ya kulala. Mbali na misaada mbalimbali inayopelekwa na wafadhili, kituo hicho kina changamoto ya eneo la kutosha la kuweza kuhifadhi watoto wengi na wa jinsia tofauti kwani kwa sasa imewalazimu kubaki na jinsia ya kiume tu kutokana na ukosefu wa vyumba vya kutosha kwaajili ya watoto hao.

Katika kuadhimisha mwezi mtukufu wa Ramadhani na ikiwa ni wiki ya kuelekea sikukuu ya Eid Al-Fitr, wafanyakazi wa Benki ya I&M waliamua kujitolea vitu hivyo katika kituo cha kulea watoto yatima Mjimwema Kigamboni ili na wao waweze kusheherekea na kufurahia sikukuu ya EID inayotarajiwa kuadhimishwa mwishoni mwa wiki hii kutegemeana na kuandama kwa mwezi. Vilevile wafanyakazi wa Benki ya I&M waliweza kuwapa elimu ya usimamizi wa fedha na ujasiriamali Vijana na Wanawake waliokuwa katika kituo hicho ili iweze kuwasaidia katika usimamizi wa fedha za kituo hicho pamoja na kujiajiri wao wenyewe pindi watakapoanza kijitegemea.

Benki ya I&M kupitia wafanyakazi wake wameweza kufanya kampeni mbalimbali za kusaidia jamii kama vile kujitolea kwa kufundisha wanawake, vijana na wajasiriamali katika kikundi cha Wanawake wajasiriami kilichopo Yombo vituka, Temeke jijini Dar es salaam, vilevile wiki iliyopita wafanyakazi wa Benki hiyo walijitolea damu  ili kusaidia wagonjwa wenye uhitaji wa damu katika Hospitali ya Taifa ya Muimbili.

Monday, May 3, 2021

I&M Holdings PLC Completes Acquisition of Orient Bank Limited in Uganda

 


 Nairobi/Kampala, 3rd May, 2021: I&M Holdings PLC has announced the majority acquisition of Orient Bank Limited (OBL) from 8 miles LLP and Morka Holdings Limited. OBL is the 12th largest bank and a licensed and established commercial bank in Uganda.
I&M Holdings PLC and Orient Bank Limited signed an agreement in July 2020 for I&M Holdings PLC to acquire 90 percent shareholding of the Ugandan entity. The acquisition was completed on 30th April 2021 after receiving the necessary approvals from the Central Bank of Kenya, Bank of Uganda, Capital Markets Authority of Kenya and the COMESA Competition Authority.
The move underscores I&M Group’s commitment to its growth and expansion strategy in Eastern Africa, where Uganda was the missing link in the Group’s strategic effort to set up its presence in all East African countries.  A key focus of this strategy is to seek opportunities to invest at a local and regional level enabling the Bank to serve the needs of all customers, while promoting trade flows within the region.
This development supports the Group’s Business Growth initiatives through diversification of revenue streams by entry into new markets and extension of its Corporate, Business, Personal Banking, as well as Treasury and Trade Finance solutions, to all its customers operating in Uganda.
Commenting on the acquisition, I&M’s Group Executive Director, Sarit Raja Shah noted, “I&M Group aspires to be Eastern Africa’s leading financial partner for growth.  The acquisition of OBL will place I&M Bank in an advantageous position to capitalise on the growth in the Eastern African economies and thereby ultimately increasing shareholder value.”
“This acquisition is expected to give the Group greater capacity to grow profitably, through extending our network to our Regional customers. Further it demonstrates our continued leadership role in the industry across East Africa”, Sarit Raja Shah added.
Dr. Ketan Morjaria, a founding member of OBL and continuing shareholder and Director said “This acquisition marks a great milestone in the history of Orient Bank. We are proud to be integrating into a regional group like I&M Holdings PLC and this synergy will allow our customers to benefit from more seamless and superior banking products whilst continuing our tradition of trust.”
Kumaran Pather, CEO of OBL said “The acquisition of OBL into I&M Holdings PLC will see the new entity rise to greater heights and allow us to broaden our market reach and penetration. The management of OBL are excited to be part of a large and
fast growing Group and look forward to serving new and existing customers alike with better products, digital platforms and regional services.”    
Through the acquisition, I&M Group has acquired additional net loan assets of approximately KES 7.7 Billion, deposits of KES 18.2 Billion, a customer base of close to 70,000, a staff component of 340 employees and a network of 14 branches and 22 ATMs across the country.
A clear plan for the integration of OBL has been developed and through its execution the Group expects to gain considerable business and operational synergies.
I&M Group has made significant investments in its robust infrastructure as part of its digital transformation journey. Through this acquisition, OBL customers will now benefit from this technologically driven infrastructure, which will give them a wide suite of market driven financial solutions aimed at meeting their financial and lifestyle requirements.  
The I&M Group will continue to focus on mergers and acquisitions as part of its growth strategy, as we continue to enhance our shareholders’ value and to provide our customers with a wide network of banking solutions across the region.
The transaction with OBL adds to a list of previous strategic alliances that the Group has effectively completed such as the acquisition of Giro Commercial Bank Limited in Kenya, I&M Burbidge Capital Limited in Kenya and Uganda, CF Union Bank in Tanzania, BCR Bank in Rwanda and First City Bank in Mauritius. We believe that our aspiration in becoming Eastern Africa’s leading financial growth partner is well on course.
In his concluding remarks, Mr. Sarit Raja Shah, noted, “Uganda has made great strides in improving access to financial services across the country. The partnership with Orient Bank Limited is very timely since the Group plans to play a significant role in the growth of the banking sector in Uganda, as it has done in other East African markets.”

Saturday, May 1, 2021

WAFANYAKAZI WA I&M BANK WAJITOLEA DAMU KUOKOA MAISHA YA WATANZANIA WAKISHIRIKIANA NA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI

 

Meneja masoko na mawasiliano benki ya I&M Tanzania kushoto Bi.Anitha Pallangyo akiwa na wafanyakazi wenzie katika kampeni ya uchangiaji dau
         Damu ikiendelea kutolewa kutokana na hamasa iliyoletwa na wafanyakazi wa Benki ya I&M
    Bi.Lencer Odhiambo kutoka kitengo cha huduma kwa wateja cha benki ya I&M akiwa anajitolea damu katika kampeni ya kuchangia damu   
    Mkuu wa kitengo cha mikopo Bw.Clemence Kagoye wa benki ya I&M akiwa anatoa damu katika kampeni ya kuchangia damu ilioandaliwa na benki hiyo

Mwandishi Wetu

Benki ya I&M Tanzania, Ijumaa tarehe 30 Aprili 2021, walifanya Kampeni ya utoaji Damu ili kuokoa maisha ya watanzania chini ya mpango wao wa ‘IM FOR YOU’ katika jitihada za kurudisha kwa jamii. Kampeni hiyo ilifanyika Makao Makuu ya Benki hiyo yaliopo Maktaba Square jijini Dar es salaam.

Zaidi ya wafanyakazi 30 walishiriki na kujitolea Damu ili kuiwezesha Serikali kukabiliana na upungufu wa Damu kupitia hospitali ya taifa ya Muhimbili ambayo ilishirikiana na Benki hiyo katika zoezi la utoaji damu.

Kwasababu uhitaji wa damu bado upo, Benki ya I&M kupitia mpango wake wa ‘IM FOR YOU’ ambao wafanyakazi wake hujitolea kwa jamii wameamua kufanya kampeni hii ya uchangiaji damu kama njia ya kurudisha kwa jamii.

Akiongea wakati wa zoezi hilo la kujitolea damu, Bi. Anitha Pallangyo, Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M alisema,”tumefurahishwa sana na muitikio ambao wafanyakazi wenzetu wameonyesha katika zoezi hili la kipekee. Tunawashukuru sana hospitali ya Taifa  Muhimbili kwa muitikio wao walioonyesha kwa kukubali kushirikiana nasi katika zoezi hili la utoaji damu ili kuokoa maisha ya watanzania wengi wenye uhitaji wa damu.”

 Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Kitengo cha Uboreshaji huduma za Benki Bi. Deepali Ramaiya, , Alisema “Hii ni moja ya mipango mikakati ya aina yake ambayo huanzishwa  na wafanyakazi wenyewe wa Benki ya I&M, kwa kujitolea huduma bure kwa jamii kama vile kutoa Elimu ya Ujasiriamali bure kwa wafanyabiashara kupitia Vikundi mbalimbali na sasa wamejitolea damu kupitia Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

 Naye Afisa muhamasishaji damu kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,John Daniel Bigambalaye alisema, “sisi kama wawakilishi wa Muhimbili kitengo cha damu, tumehamasika na kampeni hii iliyoandaliwa na wafanyakazi wa Benki ya I&M kwa jitihada hizi za kusaidia hospitali ya Taifa na watanzania wenye uhitaji wa damu kwa ujumla. Tunashauri na taasisi nyingine ziwe mstari wa mbele katika kuhamasisha wafanyakazi wake kujitolea kwa jamii”

 Benki ya I&M kupitia wafanyakazi wake wameweza kufanya kampeni mbalimbali za kusaidia jamii kama vile kujitolea kufundisha Wanawake, Vijana na Wajasiriamali, kujitolea damu  na mengine mengi kwenye sekta ya Afya, Elimu na Mazingira.

 Licha ya wafanyakazi wa Benki ya I&M kujitolea damu pia walialika Taasisi mbalimbali na kampuni zilizo karibu na Makao Makuu ya Benki ili kushiriki.